Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la watumiaji wa Huduma za Usafiri wa nchi Kavu na Majini (SUMATRA CCC), Oscar Kikoyo akizungumza wakati wa uzinduzi huo. |
Mnadhimu Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Johansen Kahatano akizungumza. |
wanafunzi wakifuatilia hotuba za uzinduzi kutoka kwa viongozi. |
Mgeni rasmi pamoja na meza Kuu ikipiga picha na Vilabu mbalimbali kutoka shule za sekondari na msingi. |
’Na Father Kidevu Blog
BARAZA la Ushauri la watumiaji wa
Huduma za Usafiri wa nchi Kavu na Majini (SUMATRA CCC), limezindua klabu ya
wanafunzi ijulikanayo kama “Sumatra Club” jijini Dar es Salaam.
Sumatra Club itakuwa inatoa mafunzo na
mbinu zitakazowawezesha wananfunzi kutambua haki zao katika huduma ya usafiri
nchini huku kauli mbiu yao ikiwa inasema, “Mtetezi wa haki, maslahi na wajibu
wa abiria”.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa klabu
hiyo uliofanyika kwenye viwanja vya sabasaba, Mwenyekiti wa Baraza hilo, Ayoob Omary amesema kuanzishwa kwa vilabu vya
Sumatra mashuleni kutasaidia kutoa elimu kwa wanafunzi ili wajue haki zao
katika huduma ya usafiri.
“Sumatra imeamua kuanzisha vilabu hivi
mashuleni ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa wanafunzi watambue haki zao katika
huduma ya usafiri na wajue namna ya kutatua matatizo wanayokumbana nayo katika
vyombo vya usafiri,” alisema Omar.
Sumatra Club vimesha zinduliwa katika
mikoa ya tisa nchini, miongoni mwayo ni pamoja na Mbeya, Mwanza, Mtwara na Dar
es Salaam na tayari wanafunzi wake wamenza kupatiwa mafunzo hayo ya haki ya
mtumiaji wa vyombo vya usafiri nchi kavu na majini.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri
la watumiaji wa Huduma za Usafiri wa nchi Kavu na Majini (SUMATRA CCC), Oscar
Kikoyo amesema mara nyingi watumiaji huduma za usafiri wamekuwa wakinung’unika
ilhali wanapaswa kulalamika maana manung’uniko hayafiki popote.
“Wanafunzi nimiongoni mwa wadau na
watumiaji wakubwa wa usafiri hasa wan chi kavu na wamekuwa wanung’unikaji
wakubwa kwa muda mrefu lakini sasa
tunataka wawe walalamikaji kwa kufuata sheria na haki walizonazo katika huduma
za usafiri,Alisema Kikoyo.
Mnadhimu Mkuu wa Kikosi cha Usalama
Barabarani, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Johansen Kahatano amesema jeshi la
polisi kwa kushirikiana na Sumatra pamoja na wanafunzi wenyewe wataweza
kumaliza changamoto ya usafiri kwa wanafunzi kama vilabu hivi vitasimamiwa
vizuri.
“Tatizo la usafiri kwa wanafunzi
litapungua na kuisha iwapo tutasimamia vyema vilabu vyetu. Niwaombe wanafunzi
wawe waadilifu na watiifu wa sheria, msiwe chanzo cha vurugu kwenye vyombo vya
usafiri. Kuweni watatuzi wa matatizo,” alisema Kahatamo.
Uanzishwaji wa vilabu hivi imeelezwa
kuwa ni moja ya mbinu iliyobuniwa na baraza la hilo ili kukabiliana na changamoto
ya usafiri kwa wanafunzi. Kila mkoa utakuwa na vilabu vyake vya Sumatra kwa
utaratibu utakaowekwa na mikoa husika.
Mathias Kondrad mwanafunzi wa kidato
cha tano kutoka shule ya sekondari Kibasila amesema, “Nimefurahi sana
kuanzishwa kwa vilabu hivi, tunaimani nasi sasa tutathaminiwa kama abiria
wengine. Tumekuwa tukichelewa shule kwa kukataliwa na hata kupigwa na
makondakta ili tusipande magari yao. Lakini sasa hivi tutatumia sheria kudai
haki yetu ya msingi kama abiria,” alisema Kondrad.
Post a Comment