Rais Malinzi
amesema timu ya Soka la Ufukweni haikupata matokeo mazuri katika mchezo wake
kutokana na ugeni wa michuano hiyo, uzoefu ndio ulikuwa kikwazo kwa timu ya
Tanzania, kwani ndio mara ya kwanza kushiriki michuano hiyo ikiwa ni miezi sita
tangu kutambulishwa kwa mchezo huo nchini Tanzania.
Ili kuwa na timu
bora ya Taifa na wachezaji wengi wa mchezo huo, Shirikisho la Mpira wa Miguu
nchini TFF limepanga kuutangaza na kuufundisha mpira wa ufukweni katika mikoa
mbali mbali nchini Tanzania, tofauti na sasa ambapo mchezo huo unachezwa Dar es salaam na Zanzibar.
Katika mchezo wa
jana mabao ya Tanzania yalifungwa na Ally Rabbi (3) Kashiru Salum (1), Tanzania
imetolewa kuwania kufuzu kwa fainali za Soka la Ufukweni barani Afrika na Misri
kwa jumla ya mabao 15-6.
Misri imefanikiwa
kufuzu kwa Fainali za Afrika kwa Soka la Ufukweni Visiwa vya Shelisheli,
zitakazofanyika mwezi April mwaka huu kwa mara ya saba mfululizo tangu kuanzishwa
kwa mchezo huo mwaka 2006 nchini humo.







Post a Comment