Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi.
WATU nane wamepoteza maisha na wengine 6 kujeruhiwa baada ya gari lenye namba za usajili T.599 AEG aina ya Fuso Mistubish kupinduka katika eneo la Maji mazuri, Wilayani Mbeya.


Tukio hilo limetokea leo jijini, majira ya saa mbili asubuhi katika Kijiji cha Lwanjilo Wilayani Mbeya barabara Chunya/ Mbeya.


Kamanda wa polisi Mkoani Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti kilichopo katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya.


Kwa upande wa majeruhi, Msangi alisema kuwa, watu sita wamejeruhiwa na kwamba wanapatiwa matibabu katika hospitali hiyo ya Rufaa ya Mbeya.


Kamanda Msangi ilisema, katika ajali hiyo watu saba walipoteza maisha papo hapo na mwingine wa nane aliongezeka wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya.


 Amesema, chanzo cha ajali hiyo ni kupinduka kwa Lori la mizigo ambalo lilikuwa limepakia watu na mbao likiwa katika mwendokasi eneo la maji mazuri Wilayani Mbeya kuacha njia na kupinduka.


Hata hivyo, Msangi aliongeza kuwa polisi wanaendelea na msako wa dereva wa gari hilo baada ya kufanikiwa kukimbia baada ya tukio hilo kutokea.

Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top