Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana


UONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Mkoa wa Mbeya, umeombwa, kuwachukulia hatua za kinidhamu baadhi ya viongozi wa matawi katika Jimbo la Mbeya Vijijini,ambao wamekuwa wanaoendesha  siasa za ukabila.

Kauli hiyo imetolewa jana na wafuasi wa CCM, wakati wakizungumza na Jamii moja blog, ambapo wamesema, viongozi hao wa matawi wamekuwa wakiendesha kampeni za chini kwa chini, zenye mlengo wa kuwabeba baadhi ya watu walionyesha nia ya kugombea nafasi za udiwani na ubunge, huku wakitumia silaha ya ukabila.

Walisema,chama kinapaswa kuliona hilo na kuchukua hatua za haraka kwani siasa za kupakana matope,ubaguzi dini, rangi na ukabila zimepitwa na wakati.

Alisema, Jimbo la Mbeya vijijini limekuwa na sifa kubwa ya ukabila lakini sifa hii imekuwa ikienezwa na viongozi wa kisiasa na si wananchi ambao wao wamekuwa wakivitegemea vyama hivyo kuwapelekea viongozi wenye sifa.

 Aidha, alikitaka chama hicho kutoa nafasi kwa vijana kuliongoza Jimbo hilo na kuachana na dhana za kizamani za kuwapa kipaumbele wazee ambao tena ni wastaafu wa serikali ambao tayari wamelitumikia taifa hili.

“Chama kwa sasa kinatakiwa kuwalea wazee haona kuwatunza kwani niamana kwa Taifa katika kutoa ushauri lakini si kushika uongozi,”alisema.

Mwisho.


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top