Mchungaji
Kiongozi wa Kanisa la Uzima na Ufufuo, Josephat Gwajima amejisalimisha
kituo cha polisi kati kuhojiwa juu ya kutoa lugha chafu dhidi ya Askofu
Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp
Kardinali Pengo. Mchungaji Gwajima anadaiwa kumkadhifu na
kumtukana hadharani Kardinali Pengo. Inadaiwa matusi hayo yameonekana
kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii ya WhatsApp na mingineyo, ambapo
kuna sauti iliyorekodiwa na picha za video zikimuonyesha Mchungaji
Gwajima akimkashifu na kumtukana kwa maneno makali Kardinali Pengo
katika hali ambayo pia imewaudhi watu wengine. |
Post a Comment