Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila (wa pili kushoto) akikabidhi cheti cha shukrani kwa  Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Kusini, Salema Kileo kutokana na udhamini wa benki hiyo katika maonyesho ya mifuko ya uwezeshaji, programu na vikundi vya kifedha yaliyoandaliwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) katika hafla ya ufungaji rasmi wa maonyesho hayo katika Viwanja vya Ruanda Nzovwe mjini Mbeya leo. Kushoto ni Katibu Tawala wa mkoa huo, Mariam Mtunguja.

Mkuu wa Uhai wa Wateja wa NBC Tanzania, Gaudence Shawa (kulia) akizungumza na Mshauri wa Kilimo na Huduma za Fedha Vijijini wa Mfuko wa Kuendeleza Sekta ya Fedha Tanzania (FSDT), Samora Lupalla (katikati) huku Ofisa Habari wa mfuko huo, Victor Kyando akiangalia katika hafla ya ufungaji rasmi wa maonyesho hayo katika Viwanja vya Ruanda Nzovwe mjini Mbeya leo. Kushoto ni Meneja Mahusiano wa NBC Tanzania, William Kallaghe.

Baadhi ya wafanyakazi wa NBC Mkoa wa Tawi la Mbeya wakihudhuria hafla ya ufungaji wa meonyesho hayo katika Viwanja vya Ruanda Nzovwe mjini humo leo.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top