| Mkuu wa kitengo cha Oparesheni Tanesco Mbeya Daud Mkotya |
| Gari lilotumiwa na Mtuhumiwa huyo katika harakati zake |
| Mafundi Tanesco wakikata umeme ulioibiwa na mtu huyo |
| Meneja Tanesco Mkoa wa Mbeya Enginia Amos Maganga |
Hatimaye Shirika la Ugavi wa Umeme Tanesco Mkoa wa Mbeya,
limefanikiwa kumkamata mtu mmoja ambaye
inadaiwa kuwa ni Mwizi wa mafuta ya Transifoma kwa kipindi kirefu sasa.
Mbali na kuhusika na wizi huo, pia mtu huyo ambaye
maharufu kwa jina la kishoka, inasemekana amekuwa akijitambulisha kuwa yeye ni
injinia kutoka kwenye shirika hilo hivyo, amekuwa akiwaunganishia watu umeme na
kuwatoza kiasi cha fedha.
Tukio hilo limetokea jijini Mbeya Mei 20 mwaka huu majira ya saa10:30 za jioni katika eneo la
Ituha Sae lililopo Jijini Mbeya, ambapo watumishi wa shirika hilo
wakishirikiana na askari polisi walifanikiwa kumbaini mtu huyo
na kumtia nguvuni.
Mkuu wa usalama wa
Mkoa Tanesco, Cyprian Lugazia, amemtaja mtu huyo kuwa ni Daniel Mwantika ambaye
amekuwa akilisumbua shirika hilo kwa muda mrefu sasa.
Amesema, mbali na hilo kishoka huyo amekuwa
akijitambulisha kuwa yeye ni injinia wa umeme kutoka shirika hilo hivyo
huwachukua vijana na kufungua transfoma
na kuiba mafuta hali ambayo imekuwa ikilighalimu shirika ikiwa na jamii kukosa
umeme kutokana na kuungua hovyo kwa transfoma hizo.
Amesema shirika hilo lipo kwenye oparesheni ya kuwabaini
wahujumu wa nishati ya umeme na mafuta ya transfoma baada ya kushamiri kwa
vitendo hivyo na kulitia hasara ya mabilions ya fedha shirika.
Amesema wakati wapo katika masako huo walifanikiwa kupata
taarifa ya mtu huyo amekuwa akilihujumu shirika kwa kuiba umeme nyumbani kwake
na pia amekuwa akiwasambazia majirani wa eneo hilo na kuwatoza fedha pamoja na
kuchukua malipo ya ankra.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Tonya Ituha Kata ya Ilomba Ndugu
Jackson Mdemwa amesema tukio hilo la kukamatwa kwa mhalifu huyo nik tukio la
kwanza kutokea katika eneo hilo.
Kufuatia wizi huo Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mbeya Enginia
Amos Maganga Amesema Katika kipindi cha
mwaka mmoja shirika hilo limepata hasara
ya shilingi milioni 600 kutokana na kuungua kwa transfoma 12 huku wizi wa umeme
ukigharimu kama milioni 400.
Amesema, uharibifu wa miundombinu wa shirika la umeme
umeendelea kukua kwa kasi kubwa hivyo ameiomba jamii kutoa ushirikiano na
kwamba kutokana na tukio hilo shirika limemsimamisha kazi kibarua ambaye
alikuwa na jukumu la kusoma mita katika eneo hilo.
Mwisho.






Post a Comment