| Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro |
Kutokana na Kushuka kwa bei ya zao la kahawa katika soko la Dunia jumla ya
Halmashauri Nne za Mkoa wa Mbeya zimetajwa kushuka kiuchumi katokana na kuibuka
kwa hali hiyo.
Halmashauri zilizo athirika ni pamoja na Halmashauri ya
Wilaya ya Ileje ,Halmashauri ya Mbeya ,Mbozi
na Rungwe ambazo kwa kiwango kikubwa zimekuwa zikitegemea zao hilo
katika moja ya pato lake.
Katika Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndugu Abbas
Kandoro ikielezea mpango wa utekelezaji
wa matokeo makubwa sasa BRN hususani katika
sekta ya kilimo mkuu huyo wa Mkoa amesema hatua ya kushuka kwa bei ya zao la
kahawa katika soko la dunia kumeshusha kwa kiwango kikubwa makusanyo katika
halmashauri hizo.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa bei ya kahawa katika
soko la dunia ilishuka kutoka
shilingi 4,000 hadi 1000 kwa kilo hali
ambayo iliwadhohofisha kwa kiwango kikubwa wakulima wa zao hilo.
Amesema katika halmashauri ya Mbozi pekee imeathiriwa zaidi
na hali hiyo hasa kutokana kutegemea
ushuru wa kahawa.
Amesema katika makusanyo ya sasa 2013/14 Halmashauri hiyo
imekusanya Tsh,645,206,757.7 ambayo nisawa na asilimia 32 tu ya lengo la kukusanya Tsh,2,000,000,000.00/ kwa mwaka.
Kufuatia hali hiyo
halmashauri hizo hususani Mbozi zimetakiwa kuimarisha ukusanyaji kutoka vyanzo
vingine sanjali na kubuni vyanzo vipya vya mapato.
mwishoo.








Post a Comment