Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Gullam Husein Kifu mwenye shati la Drafti aliyesimama


Na EmanuelMadafa,Mbeya
Wafanyabiashara wa zao la Mpunga Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya Wamegomea halimashauri hiyo kwa hatua yake ya kupitisha uamuzi wa kutoza tozo mpya kwa zao hilo  kutoka shilingi 1000 hadi 2000.

Hatua hiyo inakuja kufuatia Halm ashauri hiyo kupitia baraza lake la Madiwani kupitisha azimio la kuanza kutoza tozo mpya kwa wafanya biashara wa zao hilo kutoka shilingi 1000 hadi shilingi 2000.

Pia mgomo huo wa Wafanyabiashara  unatokana  na baadhi ya watendaji wa  Halmasahuri hiyo kuwatoza ushuru wafanyabiashara hao mara mbili kinyume na taratibu.

Akizungumza wilayani  Wilayani  humo mkuu huyo wa wilaya  ameonyesha kushangazwa na hatua hiyo ya wafanyabiashara kugomea agizo hilo licha ya Halmashauri hiyo kupitia baraza lake madiwani kupitisha azimio hilo .

Amesema kumeibuka kwa kundi la baadhi ya watu ambao wamepanga mkakati wa kutaka kukwamisha mpango huo kwa lengo la kuhakikisha halimasahuri hiyo inasahindwa kujiendesha.

Amesema kwa asilimia kubwa halimasahuri hiyo inategema pato lake kutoka  kwenye kilimo hususani kilimo cha mpunga hivyo kukwama kwa zaoezi hilo kutachangia kwa sailimia kubwa Halmashauri hiyo kushindwa kijiendesha.

Kufuatia hali hiyo Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wafanyabiashara hao kuketi pamoja na kulijadili suala hilo badala ya kuendelea kuleta msuguano  usio na tija kwa msakabari wa Halmashauri hiyo.

Hata hivyo Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Rujewa Ndugu Festo Mkemwa amesema kuwa hatua ya wafanyabiashara hao kugoma kulipa tozo hiyo mpya ya shilingi 2000 ni kukiuka sheria.

Pia amesema mgomo unaibuka wakati teyari mamlaka hiyo  kupitia baraza lake la madiwani limekwisha tunga sheria ndogo toka mwaka jana ikiambatana  na utolewaji wa  elimu kwa wafanyabiashara hao pamoja na wananchi kwa ujumla.
Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top