Kamanda wa Polisi Mbeya Ahmed Msangi |
Na EmanuelMadafa
Jeshi la Polisi
Mkoani linamshikilia Mkazi wa kijiji cha Lusungo Wilayani Kyela Mkoani Mbeya
Ndugu Obedi Makupa(37 )kwa tuhuma za kuiba mtoto mchanga mwenye umri wa siku
tano aitwaye David Semen.
Tukio hilo
limetokea June27 mwaka huu majira ya saa 04:00 alfajiri katika kijiji hicho
cha Lusungo Wilayani Kyela.
Inadaiwa kuwa
mtuhumiwa kabla ya kutenda kosa hilo aliwavizia wazazi wa mtoto huyo ambao ni Semeni Ogada (28) naTumpale Sakwisya (20) wote wakazi wa
kijiji cha lusungo wakiwa wamelala usingizi na kufungua mlango wa nyumba
uliotengenezwa kwa matete kisha kumuiba mtoto na kukimbia nae.
Hata hivyo baba
wa mtoto alishtuka na kupiga kelele za kuomba msaada hivyo majirani
walijitokeza na kumkimbiza mtuhumiwa na kumkamata akiwa na mtoto huyo.
Mtuhumiwa amejeruhiwa baada ya kushambuliwa kwa kupigwa sehemu mbalimbali za
mwili wake na wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi.
Mtuhumiwa
aliokolewa na askari polisi waliofika eneo la tukio na amelazwa hospitali ya
wilaya ya kyela akiwa chini ya ulinzi. Aidha mtoto amefanyiwa uchunguzi wa
kitabibu na kukabidhiwa wazazi akiwa salama.
Post a Comment