![]() |
| Afisa Usalama Tanesco Mkoa wa Mbeya Ciprian Lugazia akitoa ufafanuzi juu ya kuwepo kwa wateja waliounganishiwa umeme na Kishoka . |
![]() |
| Nguzo ya shirika la Mawasiliano TTCL ikiwa imetumika kama sehemu ya nguzo ya umeme kusambazia wateja feki. |
Picha na jamiimojablog
Na EmanuelMadafa.Mbeya
WATU wanne wanashikiliwa na Shirika la Ugavi wa
Umeme nchini (Tanesco) Mkoa wa Mbeya,kwa tuhuma za kulihujumu shirika kwa
kujiunganishia kinyume cha utaratibu.
Hatua hiyo imekuja zikiwa zimepita wiki mbili tangu
shirika hilo kumkamata mkazi wa Ituha, Jijini hapa, Daniel Mwantika kwa tuhuma
za kuliibia umeme shirika hilo na kuusamba kwa majirani zake huku
akijitambulisha kuwa ni injinia wa shirika hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa kitengo
cha usalama Mkoani Mbeya, Cyprian Lugazia, alisema watu hao wanne walikamatwa
katika maeneo tofauti Jijini hapa ambayo ni
Songwe, Ilomba, Kagera na Ituha.
Lugazia, ingawa hakuwa tayari kuwataja majina watu
hao kwa kuwa uchunguzi bado unaendelea , alisema zoezi hilo lilifanikiwa
kutokana na taarifa za wasamalia wema.
Meneja wa Tanesco mkoa wa Mbeya, Injinia Amos
Maganga, akizungumzia tukio hilo, amesema kutokana na hujuma hizo, shirika la
Tanesco kwa kipindi cha miezi sita shirika hilo limepata hasara ya shilingi
bilioni moja.
Mei 20 mwaka huu Tanesco Mkoa wa Mbeya, lilimkamata
Mwantika likimtuhumu kujiunganishia umeme kinyemela na majirani zake na tayari
amefikishwa mahakamani.
Mwisho.











Post a Comment