Ndugu wa askari Neema wakijaribu kumficha mtuhumiwa huyo ili asibambwe na kimulimuli chetu |
watuhumiwa wakirudishwa rumande |
Na
EmanuelMadafa.Mbeya
MAHAKAMA Kuu ya
Tanzania(Mbeya), imeanza kusikiliza kesi ya waliokuwa askari polisi watatu
ambao wanadaiwa kuhusika na mauaji ya
aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Teofile Kisanji
(TEKU) Daniel Mwakyusa.
Waliofikishwa
Mahakamani mbele ya Jaji Temba kwa kesi namba 26/2013 ni pamoja na Askari F
5842 DC Maduhu,F 7769 DC Shaban na WP 6545 DC Neema ambao wanatetewa na wakili
wa kujitegemea Mika Thadayo Mbise.
Akisoma
mashitaka hayo, Wakili wa Serikali, Hashim Ngole, aliiambia Mahakama hiyo,
watuhumiwa wote kwa pamoja walihusika na mauaji ya Daniel Mwakyusa February 14
mwaka 2012 ambapo watuhumiwa wanadaiwa kumpiga marehemu huyo kwa kutumia silaha
inayodhaniwa kuwa ni bunduki nje ya ukumbi wa starehe
ujulikanao Univesal uliopo Uyole jijini Mbeya.
Aidha,
watuhumiwa wote walikana mashitaka yao, ndipo wakili upande wa
serikali alianza kuwaongoza mashahidi watano kutoa ushahidi
mahakamani hapo chini ya kiapo huku Jaji akisaidiwa na wazee watatu wa
Baraza ambao ni Agry Ngao,Sheria Mwakatumbula na Pilly Mwakatundu.
Shahidi
wa kwanza katika kesi hiyo alikua ni Daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa
marehemu huyo kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya Dkt.Yunusi Mbaga, ambaye
aliimbia mahakama kuwa kifo cha marehemu kilitokana na kuvuja damu kwa wingi
katika mapafu na moyo wake.
Amesema,
kuvuja kwa damu huko kulitokana na majeraha yanayodhaniwa kuwa ni ya risasi
ingawa katika uchunguzi baada ya upasuaji mwili wa marehemu hakukutwa na risasi
yoyote licha ya kuwepo kwa uthibitisho wa matundu sita ya risasi
kwenye mwili wake.
Akitoa
ushahidi wake shahidi wa pili ambaye alikua ni muuguzi wa zamu katika hospitali
ya Rufaa ya Mbeya ambaye alijitambulisha kwa jina
la Sivian, alisema yeye aliupokea mwili wa marehemu Daniel February
14 mwaka 2012 usiku na kuuhifadhi kwenye chumba cha kuhifadhia maiti.
Akielezea
utaratibu wa hospitali wa kupokea miili ya marehemu, Muuguzi huyo alisema
muuguzi wa zamu anapaswa kupokea maiti usiku kutoka kwa askari polisi kwa
kuzingatia taratibu husika ikiwemo ya wahusika ambao watahusika na mwili huo
kujaza fomu husika lakini kwa siku hiyo jambo hilo halikufanyika.
Muuguzi
huyo, aliendelea kufafanua kuwa yeye akiwa amemaliza kuhifadhi mwili huo na
kukifunga chumba hicho, matumaini yake yalikuwa ni kuwakuta askari hao nje
wakisubiri kujaza fomu hiyo lakini cha ajabu wakati akitoka nje alishangaa
kutowaona wahusika hao.
Kwa
upande wake shahidi wa tatu, ambaye ni mfungwa katika Gereza la Ruanda lililopo
Mkoani Mbeya, Otieno Edward, ambaye aliimbia mahakama ya kuwa siku ya tukio
yeye alikuwa ni mlinzi wa kumbi hiyo ya starehe na kueleza jinsi ya tukio
lilivyotokea.
Mbali
na hilo shahidi huyo alitumia nafasi hiyo kuiambia mahakama ya kwamba kutokana
na yeye kuwa shahidi katika kesi hiyo, jeshi la polisi limembambikia
kesi ya wizi wa kutumia silaha hali iliyopelekea kutumikia kifungo
cha miaka 30 jela.
Baada
ya kusikiliza malalamiko ya shahidi huyo Jaji, alimwagiza Wakili wa serikali
kufuatilia suala na kupatiwa ufumbuzi haraka iwezekanavyo.
Kesi
hiyo inaendelea kusikilizwa mahakamani hapo na kwamba Shauri hilo limevuta hisia za watu
wengi na kufanya ukumbi wa Mahakama kuu kufurika mahakamani hapo.
Mwisho
Post a Comment