Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mwalimu wa shule ya Msingi Ruiwa Wilayani Mbarali mkoani mbeya Ndugu   Laiton Ngoli akiwa na wanafunzi wake  ambao ni watoto wa jamii ya wafugaji.


Masomo yakiendelea

Nje ya Darasa 






Na EmanuelMadafa,Mbeya
Serikali ya Kijiji cha  Maendeleo  Kata ya Ruiwa Wilayani Mbarali  Mkoani kwa kushirikiana na Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Ruiwa,Manfred komba, waamua  kuanzisha shule  ya msingi kinyume cha utaratibu, lengo likiwa ni kujitafutia kipato kutoka kwa wafugaji.

Aidha shule hiyo inavyumba viwili vya kufundishia pamoja na ofisi moja ya walimu imejengwa kwenye Kijiji cha Maendeleo kilichopo katika Kata ya Ruiwa na kwamba inajumla ya wanafunzi 320 kuanzia ngazi ya awali hadi darasa la sita.

Pia, watoto hao hufundishwa na Mwalimu mmoja aliyetambulika kwa jina la Laiton Ngoli ambaye aliwekwa na wananchi wa eneo hilo ambao ni jamii ya wafugaji kuwafundisha wanafunzi ngazi ya awali kutokana na shule zilizopo kujengwa mbali hivyo kuwalazimu watoto kutembea umbali mrefu wa kilomita 11 -8.

Wakizungumza na blog hii, wananchi wa kijiji hicho cha Maendeleo, walisema kutokana na jiographia ya eneo hilo kuwa mbaya hasa nyakati za mvua, iliwalazimu wao kujenga majengo hayo mawili , kisha kumuomba Mwalimu Laitoni Ngoli kuwafundisha watoto wao  elimu ya awali.

Wamedai kuwa  wakati Mwalimu huyo akiendelea kutoa elimu hiyo ya awali, inasemekana Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Ruiwa Manfred Komba kwa kushirikiana na watendaji wa serikali ngazi ya Kata na Mratibu wa elimu Kata, Joseph Mrita, walifika na wazo nzuri la kumtaka mwalimu huyo kufundisha watoto wa darasa la kwanza hadi la sita  ingawa watoto wa darasa la nne na la  sita wamesajiliwa shule ya msingi  mama ya Ruiwa.
         
Amesema, hali hiyo imewatia mashaka na kubaini kwamba viongozi hao wamekuwa wakiwachezea mchezo kwa kuchukua fedha zao ambapo inasemekana kuwa kila mfugaji amekuwa akichangia kiasi  cha fedha thamani yake ikiwa ni ng’ombe wawili hadi watatu.

Mbali, na changamoto hizo, pia wazazi hao wamehoji  ubora wa elimu inayotelewa na mwalimu huyo ambaye inasemekana  hajakidhi vigezo vya kufundisha madarasa  ya juu.

Akizungumzia hilo, Mwalimu Laiton Ngoli, alikiri  serikali ya kijiji kumpa dhamana ya kufundisha watoto hao licha ya kutambua kiwango chake cha taaluma kinaishia wapi, huku akisisistiza kwamba ameanza kufundisha darasa la kwanza na sita mwaka 2010 hadi  hivi sasa.
             
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ya msingi ya Ruiwa, alikiri Mwalimu huyo kufundisha watoto hao lakini aligoma kuzungumzia suala la usajili wa shule hiyo.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Maendeleo Charles Mkisi alisema  serikali ilitoa kibali cha wazazi kuongeza majengo ya  madarasa ya kusomea watoto kwenye eneo hilo lakini suala la usajili halifahamu.
 Kwa upande wake Afisa Elimu Wilaya ya Mbarali, Enerico Batinaluho , alisema suala hilo ndio analisikia kutoka kwa waandishi wa habari na kuhaidi  kulifuatilia.

 Hata hivyo, wazazi hao wameiomba Serikali kuingilia kati hatma ya shule ya Msingi ya Kijiji hicho  kwani msimu wa mvua umekaribia hofu yao kubwa ni ufikaji shuleni kwa watoto hao ambapo licha ya kutembea umbali mrefu bado itawalazimu kuvuka mito mikubwa miwili ya maji.

Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top