Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
(Picha Maktaba)

Na Mwandishi wetu ,Mbeya
Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linawashikilia watu watano  kwakosa la kujihusisha na biashara ya na pombe  kali zilizopigwa marufu .

Matukio ya kukamatwa kwa watu hao yamehusisha maeneo tofauti mkoani hapa ambapo katika tukio la  kwanza, Mkazi wa Mkwajuni Wilaya ya Chunya Ndugu Prisca Sinkala (31) alikamatwa  akiwa na pombe ya moshi [gongo]  yenye ujazo wa lita 05.

Mtuhumiwa alikamatwa Octoba 22 mwaka huu  majira ya saa 12 jioni huko katika  kijiji cha  mkwajuni, chunya, mkoa wa Mbeya ambapo  Mtuhumiwa ni muuzaji wa pombe hiyo

Katika tukio  la pili, Mkazi wa Soweto Mbeya  Isaya Daron (27) amekamatwa akiwa na pombe kali [viroba] zilizopigwa marufuku aina ya boss paketi 30 ambapo Mtuhumiwa alikamatwa Octoba22 mwaka huu  majira ya saa 8 mchana huko soweto.

Katika tukio la tatu, Mkazi wa airport jijini mbeya aitwaye Ndugu Salehe Sekile (32) anashikiliwa na jeshi hilo  akiwa na kete 12 za bhangi sawa na uzito wa gramu 60 ambapo Mtuhumiwa alikamatwa katika msako uliofanywa na jeshi hilo octoba  22 mwaka huu.

 Mtuhumiwa alikutwa na kete hizo baada ya kupekuliwa kwenye mifuko yake ya suruali ambapo  mtuhumiwa ni mtumiaji  na muuzaji wa bhangi hiyo.

Aidha jeshi  hilo la polisi mkoa wa mbeya linawashikilia watu wawili wakazi wa manga jijini mbeya ambao ni  Teresia Mwaisakile (31) na Elizabeth londele (29) wakiwa na pombe ya moshi [gongo] ujazo wa lita 01.

Watuhumiwa kwa pamoja walikamatwa katika msako uliendeshwa na jeshi la polisi mkoa wa mbeya ambapo taratibu za kuwafikisha mahakamani watuhumiwa hao zinaendelea.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishna msaidizi wa polisi Barakael Masaki anatoa wito kwa jamii kuacha kutumia dawa za kulevya/pombe ya moshi pamoja na pombe kali zilizopigwa marufuku nchini kwani ni kinyume cha sheria na ni hatari kwa afya ya mtumiaji.

mwisho


Mwisho.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top