Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Na Emanuel Madafa,Mbeya .
KLABU ya timu ya Tanzania Prisons imekataa ofa ya kuwauza wachezaji wao muhimu  wawili Nurdin Chono na Salum Kumenya  ili kumaliza  mzunguko wa kwanza  wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania.

Viungo hao wawili wa ushambuliaji wamekuwa gumzo ndani ya jiji la mbeya kuwa huenda wakanyakuliwa  na wekundu wa msimbazi  Simba  kupitia dirisha dogo.

Akizungumzia  hilo, Katibu wa klabu ya timu ya Prisons, Oswald Morris  alisema kikosi cha timu hiyo bado kinawahitaji wachezaji hao muhimu ili kuisukuma timu hiyo kusonga mbele tofauti na Simba wanavyofikiria.

Amesema, wiki iliyopita uongozi ullipokea simu kutoka kwa uongozi wa Stendi United, ukimtaka mchezaji Ibrahim Mamba lakini hakuna barua iliyowasilishwa mezani.

“Prisons imekuwa ikiingia mkataba na wachezaji kwa miaka miwili hivyo mpaka sasa tunazaidi ya mwaka mmoja wa kuwamiliki wachezaji  wetu,”alisema.

Hata hivyo, Katibu huyo alisema kuwa kikosi cha Prisons kikiwa na wachezaji wake wote, kinatarajia kuingia kambini November 23 mwaka huu. 

Mwisho. 

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top