Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Na EmauelMadafa , Michuzi Blog , MBEYA.

MIGOGORO ya wazazi katika familia, imetajwa kuwa ni moja ya sababu kubwa inayoathiri elimu na malezi bora ya watoto.

Kauli hiyo imetolewa jijini Mbeya na Afisa  Utawala Shule za St.Mary's Mkoa wa Mbeya, Anuciata Ngonyani kwenye mahafali ya wanafunzi 63 wa darasa la saba.

Amefafanua  kuwa uongozi wa shule hiyo umekuwa ukipokea kesi nyingi za namna hiyo, hivyo kuwaomba wazazi wakiume kutambua wajibu wao kwa watoto ikiwa na kuwatendea haki kwa kutimiza haki zao za msingi ikiwemo elimu.

Aidha, amewataka  wazazi kujenga mshikamano, umoja, amani na upendo kwenye familia ili watoto waweze kuiga mambo yaliyomema na kukua katika maadili.

Amesema kuna watoto wengi wameacha masomo na wengine kuhamishwa  shule  kutokana na jukumu la kusomesha mtoto kuachiwa mama pekee jambo hali ambayo imekuwa ikimnyima haki mtoto.  .

 Kwa upande wake Meneja wa bima Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Consolatha Gabone amesema moja ya changamoto zinazo poteza ndoto za watoto ni mifarakano ndani ya familia hasa pale wazazi wanapo tengana au kufariki.

Amesema kutokana hali hiyo wameamua kuanzisha huduma ya bima ya maisha ambayo inatoa fursa kwa wategemezi kutimiza ndoto zao bila kuathiri mfumo wa maisha licha ya kuondokewa na wazazi.

Gabone amesema kuwa imekuwa ni jambo la kawaida kwa wazazi kuwa na bima za magari na mali nyingine na kusahau bima za maisha ikiwemo elimu ambayo ni njia ya kumwezesha mwanafunzi kufikia ndoto zake kabla ya kuanza kujitegemea.

Amesema ili kuweza kuonyesha upendo kwa watoto ni vema wakafungua bima ya elimu ili kuweza kutimiza malengo ya watoto.

Wengi wamesau kwa habari ya maisha yao wenyewe  unajua mzazi anapo kuwa amekata bima ya maisha ni kuonyesha upendo kwa familia lakini kuna wakati unaweza kupata madhara hivyo ukashindwa kusomesha lakini ukakata bima hasa ya elimu watoto wataendelea na masomo hivyo niwashuri wazazi kukata bima ili kuwezesha kutimza malengo ya watoto wao’alisema Gabone

 
Afisa  Utawala Shule za St.Mary's Mkoa wa Mbeya, Anuciata Ngonyani akizungumza kwenye mahafali ya wanafunzi 63 wa darasa la saba.

Wahitimu wa elimu ya msingi darasa la Saba katika shule ya St.Merys Mbeya wakiwa makini kumsikiliza  Afisa  Utawala Shule za St.Mary's Mkoa wa Mbeya, Anuciata Ngonyani katika shehere za mahafali ya 63 ya shule hiyo.

Rose Lwakatare (Mtoto wa Mchungaji Mama Lwakatare ) akizungumza katika sherehe hizo zilizofanyika shuleni hapo .

Meneja wa bima  (TIRA)Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Consolatha Gabone  akizungumza katika mahafali hayo 


Wanafunzi wakitoa burudani katika sherehe hizo.

Wazazi na Walezi ambao walipata fursa ya kuhudhuria sherehe hizo 



Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

 
Top