Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Meneja wa kituo cha Utafiti cha TacrI  cha Mbimba Mbozi Kushoto Ndugu Isack Mushi akitoa maelezo ya kitafiti mara baada ya kutembelewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda (hayupo pichani ) katikati  ni Naibu Waziri Kilimo Ushirika na Chakula Godfrey Zambi pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro kulia.


Na Mwandishi wetu,Mbozi
Kituo cha utafiti wa zao la kahawa cha TacrI Kanda ya Nyanda za juu kusini Mbeya na Katavi kimeendelea na juhudi mbalimbali zaa kuhakikisha kinaongeza zaidi   ubora wa kahawa kutoka daraja 9,13 hadi 5 na 9.


Akizungumza  Meneja kituo hicho  cha utafiti wa zao la kahawa kilichopo Mbimba Mbozi Ndugu Isack Mushi amesema katika kufikia lengo hilo kituo hicho kimenza na jitihada za kuongeza uzalishaji kwa mti wa kahawa kutoka gramu 250 hadi kufikia walau gramu 1000 ambayo ni sawa na kilo moja.


Amesema hatua nyingine ni kuongeza uzalishaji wa miche bora ya kahawa ili kukidhi mahiyaji ya wakulima sanjali na  kukagua rutuba ya udongo wa maeneo ya kahawa na kutoa mapendekezo muafaka ya urutubishaji.


Aidha Meneja huyo amesema kuwa zipo changamoto mablimbali ambazo kituo hicho kinakabiliana nazo ambazo ni pamoja na kuwepo kwa ufinyu wa bajeti ya utafiti kutoka serikalini.


Amesema changamoto nyingine ni uwekezaji hafifu wa halmashauri za wilaya katika kuendeleza kilimo cha kahawa.


Kutokana na changamoto hizo Meneja huyo ameitaka serikali kuhakikisha inaongeza bajeti yake katika kugharamia shughuli za utatifi wa zao hilo.



Awali katika ziara yake hivi karibuni  Wilayani Mbozi Mkoani Mbeya Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliwataka maafisa kilimo katika halmashauri hiyo kutoa elimu kwa wakulima wa zao hilo kuhakikisha wanaendeleza kilimo hicho kwa kufuata taratibu bora za kilimo hicho.
 
Alisema kuwa kwa mwaka 2014 ,15 zao hilo la kahawa kwa wakulima liliwaingizia zaidi ya shilingi bil30 hivyo kama wakulima
Zao la kahawa likiwa shambani
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akifuatilia maelezo toka kwa Meneja wa kituo cha Utatifi cha TacrI  Ndugu Isack Mushi mara baada ya kutembelea kituo hicho hivi karibuni kituo ambacho kinahudumia mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Mbeya na Katavi.JAMIIMOJABLOG

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0759 406 070

Post a Comment

  1. Government should put much efforts to support this sector in order to push up sector further for coffee

    ReplyDelete

 
Top