![]() |
Naibu waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi Mhandisi Atashasta Nditiye pili kushoto akisikiliza maelezo kutoka kwa mafundi ya karakana ya Reli ya Tazara iliyopo katika kituo cha Iyunga Jijini Mbeya |
Home
»
»Unlabelled
» NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI ATAKA WANAO HUJUMU SHIRIKA LA RELI WACHUKULIWE HATUA
Na EmanuelMadafa,Mbeya
Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi
Atashasta Nditiye amewaagiza askari polisi kitengo cha reli kuwakamata watu
wanaotuhumiwa kupiga mawe treni pindi zinapopita kwenye maeneo yao na
kuhasababisha uharibifu ambao huigharimu serikali pesa nyingi katika
matengenezo vingine watawajibishwa wao
Hayo
yameelezwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi. Atashasta Nditiye,
alipotembelea Kalakana ya Tazara iliyopo Jijini Mbeya.
Amesema
wapo baadhi ya watanzania wamekuwa wakiendelea
na vitendo vya kuhujumu treni hivyo lazima wachukuliwe hatua kali ili kukomesha
vitendo hivyo kwa kuhakikisha zinatolewa adhabu kali kwa watako bainika kufanya
vitendo hivyo.
Waziri Nditiye amewataka madereva wa treni kusimamisha treni endapo
itatokea kuna baadhiya watu wamefanya tukio la kupiga mawe treni mara iwapo
safarini ili wahusika wakamatwe na
kuhojiwa ili watoe sababu za kufanya kitendo hicho sanjali na kuchukuliwa hatua
mara mora .
Wakati
huo naibu Waziri , amewahakikishia wanyabiashara na
wachuuzi kuwa hatua ya uimarishaji wa usafiri na usafirishaji kupitia Reli
nchini,uko pazuri na tayari muda wa kuondoa mizigo mizito inayotumia malori
umefika
Amesema,katika
kuimarisha usafiri huo, zaidi ya shilingi bilioni 10 zimetolewa na serikali
kuboresha vichwa vya magari moshi na kalakana mbalimbali nchini.
Amesema,
serikali haitegemei kuona malori ya kiendelea kusafirisha mizigo mizito ambapo
wakati mwingine yamekuwa chanzo cha kuharibu miundombinu ya barabara pamoja na
kuua soko la Tazara.
“Barabara
hizi zimejengwa kwa gharama kubwa sana, tunategemea mizigo hiyo kuanza
kusafirishwa kwa kutumia njia ya reli na kwamba ni jukumu la wafanyakazi kuanza
kuwashawishi wateja wao wazamani na wapya ili wafanye kazi na
Tazara,”amesema.
Hata
hivyo amesema ,serikali haiwezi kuendelea kuwalipia mishahara lazima itafika
pahala ambapo itasitisha na kuiacha Tazara iendelee na majuku yake kwa
kujiendesha yenyewe, hivyo wanapaswa kujipanga kwa kuwa wabunifu.
mwisho.
Recent Posts
- MKUU WA WILAYA YA CHUNYA AAHIDI KUPAMBANA NA WAFUGAJI WAHALIBIFU WA VYANZO VYA MAJI07 Nov 20181
Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya Meryprisca Mahundi (katikati) akimkisikiliza kwa makin...Read more ?
- 25 Oct 20180
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila (wa pili kushoto) akikabidhi cheti cha shukrani kwa ...Read more ?
- 25 Oct 20180
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila (wa pili kushoto) akikabidhi cheti cha shukrani kwa ...Read more ?
- MHAGAMA AAGIZA NEEC KUFANYA TATHIMINI YA UHALISIA WA WANUFAIKA WA MIKOPO INAYOTOLEWA NA TAASISI ZA KIFEDHA20 Oct 20180
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenis...Read more ?
- MK17 Oct 20180
Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhandisi Meryprisca Mahundi (kushoto) akisikiliza meelezo kutoka kwa mmoj...Read more ?
- BABA AMUUA MTOTO WAKE KWA SUMU MBEYA31 Aug 20180
Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.